Ulomi aliyepotea mwili wake wakutwa Hospitali ya Mwananyamala

  

Mfanyabiashara Daisle Simon Ulomi, aliyeripotiwa kupotea tangu Desemba 11, 2024 imebainika amekufa na mwili wake inasemekana umekutwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Baba mkwe wa Ulomi, Japhet Munisi amenukuliwa akisema alipigiwa simu leo asubuhi na mke wa marehemu, akimjulisha kuwa amepata taarifa kuwa mwili wa mumewe upo hospitali hiyo. 

Mfanyabiashara huyo aliyekuwa akifanya biashara za fedha za mitandao ya simu maeneo ya Sinza Kijiweni na Mwenge alipotea tangu Tarehe 11 Desemba 2024.

Hata hivyo Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam bado halijatoa taarifa rasmi kuhusiana na kupatikana kwa mwili wa Ulomi. 

Awali Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam lilisema Desemba 12, 2024 katika kituo cha Polisi Chang'ombe, Temeke ilipokelewa taarifa ya kutafutwa na familia yake mtu aitwaye Daisle Simon Ulomi, mfanyabiashara ambaye hakurudi nyumbani kwake tangu alipoingia kazini kwake Desemba 11, 2024.

Chapisha Maoni

0 Maoni