Waziri Mkuu
Mstaafu Jaji Joseph Warioba, ametahadharisha hatua ya Jeshi la Polisi kuanza kuingizwa
kwenye siasa, na kuonya kuwa kitendo hicho ni hatari kinaweza kuwagawa
wananchi.
Jani Mstaafu
Warioba ametoa kauli hiyo leo Desemba 4, 2024 alipozungumza na Wahariri na Waandishi
wa habari jijini Dar es Salaam, na kusisitiza vyombo vya dola visiingizwe kwenye
mambo ya siasa.
“Katika
miaka michache iliyopita tumeliingiza Jeshi la Polisi kwenye siasa, na jeshi
nalo limekuwa linatoa matamko ya kisiasa na hii italeta mgawanyiko,” alisema
Jaji Mstaafu na kuongeza,
“Wananchi
watagawanyika. Kuna wale watakaoona, Jeshi la Polisi ni adui, tusifike huko.
Tuliache Jeshi la Polisi lifanye kazi zake za kawaida.”
Amesema
kwamba sasa hivi inapofika wakati wa uchaguzi vyombo vya dola vinaandaliwa kwa
ajili ya kukabiliana na ghasi, “Uchaguzi sasa umekuwa kama jambo la hatari,
haipaswi kuwa hivyo.”
Jaji Mstaafu
Warioba ambaye alikuwa akitoa maoni yake kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa
uliomalizika, amesema kuwa ulikuwa na kasoro na kasoro hizo zinapaswa
kurekebishwa.
“Uchaguzi
huu umeharibiwa na wasimamizi ambao waliwawekea mapingamizi wagombea jambo
ambalo ni kinyume, kwani wanaopaswa kuwekeana mapingamizi ni wagombea wenyewe,”
alisema Jaji Mstaafu Warioba.
Pia, amedai
kuwa wasimamizi wa uchaguzi walishiriki katika kuweka kura feki na cha
kushangaza hadi sasa Serikali imekaa kimya haijawachukulia hatu watu
walioshiriki kuharibu uchaguzi.
“Zamani
waliokuwa wakishiriki kuandaa kura feki walikuwa wagombea, ajabu sasa hivi
wanaoshiriki kuandaa kura feki ni wasimamizi wa uchaguzi,” alisema Jaji Mstaafu
Warioba akionyesha kushangaa.
0 Maoni