Tanzania imekuwa
miongoni mwa nchi zilizofanya vyema katika viwango vya soko dunia vya FIFA baada ya kupanda kwa nafasi sita kutoka
nafasi ya 112 hadi 106, na kuipita nchi ya Kenya.
Mafanikio
hayo ya Tanzania yamechangiwa na Taifa Stars kushikilia nafasi ya pili katika
Kundi H nyuma ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kufuzu kwa Fainali za
Mataifa ya Afrika 2025.
Kwa upande
wa Timu ya taifa ya Kenya ya mpira wa miguu Harambee Stars imeshuka kwa nafasi
mbili katika viwango vya hivi punde vya Fifa vilivyotolewa Alhamisi na
shirikisho hilo la soka duniani.
Timu ya
taifa ya kandanda sasa iko katika nafasi ya 108, chini kutoka nafasi ya 106
iliyokuwa nayo Oktoba.
Kushuka huku
kwa Kenya kunatokana na kushindwa kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika 2025 na
kuikosa michuano hiyo yenye hadhi ya juu zaidi barani.
Harambee Stars
ilimaliza ya tatu katika Kundi J nyuma ya Cameroon na Zimbabwe kufuatia sare ya
1-1 dhidi ya timu ya taifa ya Namibia na sare tasa dhidi ya Namibia katika
mechi mbili za mwisho za kufuzu mapema mwezi huu.
Kwa upande
wa Uganda yenyewe imesalia na nafasi yake ya juu zaidi katika ukanda wa CECAFA
licha ya kushuka kwa nafasi moja hadi 88 huku Morocco ikisalia kuwa nchi iliyo
juu zaidi barani Afrika katika nafasi ya 14.
Nchi ya Argentina
inasalia kuwa kikosi kinachoongoza juu kwenye viwango vya FIFA, huku Ufaransa
na Uhispania zikihifadhi nafasi zao katika nafasi ya pili na ya tatu mtawalia.
0 Maoni