Dkt. Mpango anunua bond za shilingi milioni 100

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amekuwa mtu wa kwanza kununua hati fungani za Samia Infrastructure Bond, ambapo amenunua hati fungani zenye thamani ya shilingi milioni 100.

Dkt. Mpango amenunua hati fungani hizo leo akizindua rasmi Samia Infrastructure Bond, ambayo ni ushirikiano wa CRDB Bank na TARURA ikiwa na lengo la kuwezesha wakandarasi wazawa wanaotekeleza miradi ya miundombinu iliyoanzishwa kwa chini ya TARURA.

Makamu wa Rais Dkt. Mpango ametoa wito kwa wananchi, vikundi na taasisi kuwekeza kwenye hatifungani ya Samia Infrastructure Bond iliyozinduliwa leo, ikiwa na lengo la kuwezesha wakandarasi wazawa wanaotekeleza miradi iliyo chini ya TARURA.

Katika hotuba yake Dkt. Mpangoa ametaka kutolewa wa elimu ya masuala ya fedha na uwekezaji wakati akizindua Samia Infrastructure Bond iliyoanzishwa kwa ushirikiano kati ya CRDB Bank na TARURA.

Chapisha Maoni

0 Maoni