Matumizi ya pombe yaliyopitiliza
yanaweza kusababisha magonjwa ya mfumo wa fahamu kwa kuwa kemikali zilizopo
kwenye pombe zina tabia ya kuleta madhara kwenye seli za mfumo wa balansi ya
ubongo ambapo mwisho wake seli za ubongo zinaweza kufa kabisa.
Kauli hiyo imetolewa na Daktari Bingwa
Mbobezi wa Magonjwa ya Mfumo wa Fahamu MNH-Mloganzila, Dkt. Mohamed Mnacho na
kuongeza kuwa mtu akinywa pombe na kulewa maana yake anakuwa ameathiri mfumo wa
balansi ya ubongo hivyo akiendelea na tabia hiyo mara kwa mara seli za ubongo
zitakufa.
Dkt. Mnacho amebainisha kuwa mtu
aliyeathirika na changamoto za mfumo wa balansi za mfumo wa ubongo ataanza
kupata changamoto za kusahau, kutetemeka, kuchanganyikiwa na baadaye anaweza
kupata kifafa ambacho kitampelekea kutumia dawa za kifafa kila siku.
“Ni vizuri jamii ikajiepusha na
matumizi ya pombe yaliyokithiri kwa kuwa pombe ikizidi inakuwa ni sumu na
madhara yake ni ya muda mrefu na mtu akipata magonjwa haya yatokayo na athari
ya matumizi ya pombe matibabu yake yana gharama kubwa na yanatumia muda mrefu
kuyatibu,” ameongeza Dkt. Mnacho.
Ni vema kama mtu anahitaji kunywa
pombe akatumia si zaidi ya chupa moja ili kuendelea kujikinga na magonjwa
yasiyoambukiza ikiwemo magonjwa yanayoathiri mfumo wa fahamu.
0 Maoni