Marekani yatoa tahadhari ya hali ya usalama Msumbiji

 

Nchi ya Marekani imetoa tahadhari ya hali ya usalama kwa raia wake waishio nchini Msumbiji hususan waliopo katika mji mkuu wa Maputo.

Tahadhari hiyo inafuatia kuongezeka kwa maandamano katika maeneo mbalimbali mjini Maputo, kwenye barabara zinazoelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Maputo, na katika miji mingi kote Msumbiji.

Ubalozi wa Marekani mjini Maputo umewataka raia wake waishio nchi hiyo kufahamu hali hiyo ya dharura.

Hapo jana tume ya uchaguzi ilitangaza kwamba chama tawala cha Msumbiji, Frelimo, kimeshinda uchaguzi huo uliogubikwa na malalamiko na kuligawa taifa hilo.

Chapisha Maoni

0 Maoni