Robert Lewandowski ametupia wavuni
magoli mawili ndani ya dakika tatu nakuisaidia Barcelona kuichakaza Real Madrid
kwa mabao 4-0 katika mchezo wa ligi kuu ya Hispania La Liga.
Real Madrid ambayo ilikuwa ikitafuta
rekodi ya kucheza michezo 43 bila ya kufungwa inayoshikiliwa na Barcelona
ilijikuta ikitibuliwa mahesabu yao katika kipindi cha pili.
Robert Lewandowski alifungua karamu ya
magoli dakika ya 54 na kisha kutumbukiza goli la pili dakika datu baadae, huku
magoli mengine ya Barcelona yakiwekwa kimiani na Lamine Yamal na Raphinha.
Katika mchezo huo Lewandowski alikosa
nafasi mbili za kuweza kufunga hat-trick. Kwa ushindi huo Barcelona wanaongoza
ligi ya La Liga kwa tofauti ya pointi sita.
0 Maoni