Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Septemba 11, 2024
amemuwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Nane
wa Mawaziri wa Umoja wa Nchi za Afrika, Karibian na Pasifiki (OACPS)
wanaohusika na masuala ya Uvuvi, Bahari, Maziwa na Mito, kwenye Kituo cha
Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Malengo ya mkutano huo ni kuimarisha utekelezaji wa
Makubaliano yaliyofikiwa; kuimarisha utekelezaji wa vipaumbele vya kimkakati
vya umoja; kubadilishana uzoefu; kuweka mikakati ya pamoja; na kuimarisha
ushirikiano na washirika ili kuboresha usimamizi wa bahari, uchumi wa buluu, na
maendeleo endelevu ya uvuvi.
Aidha, Mkutano huo unatarajiwa kutoa mwongozo wa kimkakati kwenye vikao vya juu vya maamuzi vya Umoja wa Nchi za Afrika, Karibian na Pasifiki ili kuboresha usimamizi wa bahari, uvuvi na ufugaji wa samaki endelevu.
0 Maoni