Katika
kuadhimisha Siku ya Moyo Duniani tarehe 29/9/2024 Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) itatoa huduma za tiba mkoba zijulikanazo kwa jina la Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan Outreach Services kwa kufanya kambi maalumu ya upimaji na
matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam na mikoa ya
jirani.
Upimaji huu
utafanyika bila malipo yoyote yale kwa watoto na watu wazima tarehe
28-29/09/2024 kuanzia saa mbili kamili asubuhi hadi saa 10 kamili jioni katika
kliniki ya Taasisi ya Moyo Jakata Kikwete (JKCI) iliyopo Kawe jengo la Mkapa
Health Plaza barabara ya Tuari.
JKCI
imewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kupima afya zao ili kujua kama wana
matatizo ya moyo ili kuanza matinanu mapeka kwa anayegundulika kuwa ni mgonjwa.
Kwa taarifa
zaidi wasisliana kwa simu namna 0754578190, 07839225571 na 0674179036 Taasisi
ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) hospitali ya Dar Group.
0 Maoni