Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na
Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhwani Jakaya Kikwete, amekutana na kufanya mazungumzo na
kuwapongeza Bodi ya Ushauri wa Masuala
ya Kazi, Uchumi na Kijamii (LESCO) kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yao
wanapoelekea kumaliza muda wao wa Miaka Mitatu ya Kazi.
Pamoja na kuwapongeza Mhe. Ridhwani, ametoa rai kwa wajumbe
wa Baraza hilo kuendelea kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu ili kuhakikisha
sekta ya kazi na ajira inazingatia misingi ya kazi zenye staha kwa maslahi ya
wafanyakazi na waajiri.
Awali, Mwenyekiti wa LESCO Dkt. Samwel Nyantahe, ameishukuru
Serikali kwa kutoa ushirikiano katikia kipindi chote cha utekelezaji wa
majukumu yao.
Uongozi wa Baraza hilo unamaliza muda wake Septemba 12, 2024 na kwa sasa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imeanza mchakato wa kuwapata wajumbe wengine
0 Maoni