Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kwela, Mhe. Deus Sangu
amewahakikishia wananchi kuwa atafanya kazi kwa weledi na uaminifu wa hali
ya juu huku akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa heshima kubwa aliyowapa
wananchi wa Jimbo la Kwela na Mkoa wote wa Rukwa kwa kumteua yeye kuwa Naibu Waziri wa Ofisi yake.
Aidha, Mhe. Sangu amewashukuru wananchi wote wa Mkoa wa Rukwa kwa mapokezi makubwa waliyompa mara baada ya kuwasili Mkoani humo,
ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo.
Mhe. Sangu ametoa
kauli hiyo kwa nyakati tofauti wakati
akizungumza na Watumishi pamoja na wananchi
katika Kata ya Kanda na Kaengesha
kwenye mikutano ya hadhara iliyofanyika
kwenye Vijiji vitano vya Jimbo la
Kwela , Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga
Mkoani Rukwa.
Amesema Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaheshimisha
wananchi wa Mkoa wa Rukwa kwa kumteua yeye ili aweze kumusaidia kuwahudumia
Watanzania katika masuala ya utumishi na utawala bora.
"Naomba niwaahidi katika najukumu yangu haya mapya
nitakuwa mnyenyekevu, mchapakazi, mweledi na mwaminifu katika kutekeleza
majukumu yangu ya kumsaidia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene " amesema Mhe. Sangu.
Ameongeza "Nawashukuru pia wananchi wa Kwela kwa
kuniamini na kunituma Bungeni ili nikawesemee changamoto zinazowakabili hii
imepelekea Rais Samia kuweza kuniona na kuniteua kushika Wadhifa huu.
Katika hatua nyingine Mhe. Sangu ametumia fursa hiyo
kumshukuru Mhe.Rais kwa kutekeleza miradi mingi ya maendeleo katika Jimbo la
Kwela ikiwemo ujenzi wa zahanati, barabara, maji pamoja na umeme.
Mhe. Mhe. Sangu amewahakikishi wananchi hao kuwa “Mambo mazuri zaidi yanakuja, Rais Samia
amesema anataka kuiona Kwela yenye nuru kiuchumi,” amesisitiza Mhe.Sangu.
Amesema Mhe.Rais anawapenda sana wananchi wake hususan wa
Mkoa wa Rukwa ndio maana ameongeza bei ya mazao ya mahindi hadi Sh.700 kwa kilo moja ili kuhakikisha
wananchi wa Kwela wananufaika kiuchumi kupitia kilimo chao.
Hata hivyo Mhe.Sangu ameowaonya wananchi wake wasithubutu
kuuza mazao yote la sivyo kufikia Mwezi Januari mwakani watakumbwa na baa la
njaa.
Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa, Mhandisi, Daudi Sebiga ametumia fursa hiyo kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Mhe.Deus Sangu kwani Mchapakazi na Mwaminifu wa kiwango cha hali ya juu sana.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Deus Sangu akizungumza na Elus Homera mara baada ya kuwasili katika mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Kata ya Kanda, ikiwa ni ziara ya kwanza tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo.
Sehemu ya wananchi wa Kata ya Kanda, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Mkoani Rukwa wakimshangilia kwa shwange Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.Deus Sangu mara baada ya kuwasili, ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo.
0 Maoni