Makundi ya watu waliojawa na furaha wamevamia mitaa
mbalimbali nchini Bangladesh, kusherehekea kujiuzulu na kukimbia nchi Waziri Mkuu aliyekaa
madarakani kwa muda mrefu Sheikh Hasina.
Watu wamekuwa wakipeperusha bendera ya taifa hilo na kucheza
juu ya vifaru vilivyoegeshwa katika Jiji la Dhaka, Shirika la Habari la AFP imeripoti.
Kituo cha runinga cha Channel24 kimewaonesha waandamanaji
wenye mihemuko wakivunja makazi ya Hasina yaliyopo Dhaka, na kuzipungia mikono
kamera huku wakiingia enao la nyumba hiyo.
Waziri Mkuu Sheikh Hasina amejiuzulu na kuikimbia nchi kufuatia maandamano ya kumpinga ambayo yamepelekea mamia ya watu kufa.
Waandamanaji 90 wameuawa siku ya jana Jumapili katika
mapambano na polisi, na kufanya idadi ya vifo kufikia watu 300 katika wiki za
hivi karibuni.
0 Maoni