Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata Amos
Lutakulemberwa Lwizamiaka (54) mkazi wa
Tegeta Wazo Kinondoni kwa tuhuma za kusambaza taarifa za uongo kwenye mitandao
ya kijamii kwamba binti aliyerekodiwa video Agosti 2024 akifanyiwa vitendo vya
udhalilishaji kwa kubakwa na kulawitiwa amekutwa amefariki dunia.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam SACP Muliro
Jumanne Muliro ameeleza kushikiliwa kwa mtuhumiwa huyo na kusema anahojiwa na
polisi kutokana na kutoa taarifa za uongo zenye lengo la kuzusha hali ya taharuki.
"Jeshi la Polisi linatoa wito watu kujiepusha na kutoa
au kuchapisha taarifa za uongo zenye malengo ya kuzusha taharuki katika jamii
kwani kufanya hivyo ni makosa lakini litaendelea kuzingatia maoni ya watu
ambayo hayakinzani na sheria za nchi," amesema kamanda Muliro.
0 Maoni