Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Julai 28, 2024 ameshiriki
katika mbio za hisani za Benki ya NBC zilizoanzia na kuishia katika uwanja wa
mpira wa miguu wa Jamhuri jijini Dodoma.
Mheshimiwa Majaliwa ameipongeza benki hiyo kwa kaundaa mbio
hizo zenye lengo la kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi
kwa wanawake.
Pia mbio hizo zimelenga kuchangia ujenzi wa chumba cha upasuaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
0 Maoni