Wapigakura Rwanda wamepanga foleni katika vituo vya kupigia
kura leo Julai 5, kumchagua rais ajaye, huku rais aliyemadarakani Paul Kagame
akitarajiwa kushinda.
Rais Paul Kagame mwenye umri wa miaka 66 ameliongoza taifa
hilo la Afrika ya kati karibu kwa robo ya karne, na amekuwa akishinda chaguzi zilizopita kwa zaidi ya asilimia 90.
Wagombea wanane waliomba kuwania urais kumg'oa madarakani
Kagame, lakini ni wagombea wawili tu waliopitishwa na tume ya uchaguzi kuwania
urais.
Wagombea wengine akiwamo wakosoaji wakubwa wa Kagame, wamezuiwa kuwania uchaguzi kwa sababu mbalimbali zikiwamo za kuwa na rekodi ya uhalifu.
0 Maoni