Baadhi ya Wananchi kutoka katika Mitaa ya Kolimba na Hombolo Bwawani Kata ya Hombolo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, wamesema uwepo wa Umeme wa Wakala wa Umeme Vijijini(REA) umekuwa na Mchango na Mchango mkubwa katika uboreshaji wa huduma za afya.
Wakizungumza kwa
nyakati tofauti baadhi ya wananchi kutoka
Kata ya Hombolo Mkoani Dodoma wamesema
umeme wa REA umekuwa na tija kubwa katika maeneo yao hasa kwenye sekta
ya afya.
“Umeme wa REA unasaidia sana hasa kuhifadhi dawa za Kinga
kwa Watoto Wachanga pia umeme huu umerahisisha uwepo wa maji ya uhakika pia
kuwa na fursa ya kila mtu kuwa na uwezo wa kuchemsha maji ya kunywa nyumbani
kwa kutumia heater maana hapo mwanzo huwezi hata kuchemsha umeme w REA
haukuwepo hivyo ilikuwa kila mtu
anapata nafasi ya kuunganishiwa kwa bei
ndogo tu na tunashukuru sana kwa kutukumbuka,” amesema Elizabeth Joseph.
Hii ni baada ya Wizara ya Afya,kwa kushirikiana na Wakala wa
Nishati Vijijini (REA) kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) katika
kutekeleza mradi wa kupambana na Magonjwa ya Mlipuko ikiwemo Kipindupindu na
Uviko-19 kusambaza umeme katika visima ambavyo havikuwa na pampu za umeme za
kuvuta maji na vituo vya kutolea huduma
za afya katika Mkoa wa Dodoma kwa Wilaya
za Dodoma , Chamwino, Bahi, Chemba, Kongwa na Mpwapwa.
Mikoa mingine inayotekelezwa na Mradi huo ni Mwanza, Kagera, Simiyu, Kagera, Arusha, Pwani, Lindi, na Mtwara.
0 Maoni