Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda
amewavisha nishani Maafisa na Askari wa Vikosi vilivyoko Kanda ya Dar es Salaam
na Pwani kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi
Mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan.
Hafla hyo imefanyika Jijini Dar es Salaam kwenye uwanja wa Mgulani leo tarehe 7 Juni 2024 kwa kuwavisha Nishani ya Utumishi Uliotukuka Tanzania, Nishani ya Utumishi Mrefu na Nishani ya Utumishi Mrefu na Tabia njema.
Wakati huo huo, Jenerali Mkunda amewavisha Nishani ya Ulinzi wa Amani ya SADC Maafisa na Askari kwa niaba ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC kwa kutambua mchango wao katika Ulinzi wa Amani nchini Msumbiji chini ya Mwavuli wa SADC iliyowatunuku Nishani hiyo.
0 Maoni