Dkt. Nchimbi ahitimisha ziara ya Arusha kwa kishindo

 

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi akizungumza na wananchi wa eneo la USA River, Wilaya ya Arumeru, Mkoa wa Arusha, aliposimama kuwasalimia akiwa njiani kutokea Arusha mjini, akihitimisha ziara ya siku tatu mkoani humo, kisha kuelekea Mji wa Bomang’ombe, Wilaya ya Hai, tayari kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani Kilimanjaro. 

Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu Balozi Nchimbi ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Komredi Amos Gabriel Makalla na Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Rabia Hamid Abdalla. 

Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo CPA Amos Gabriel Makalla akisoma moja ya mabango yanayoelezea kero za wananchi wakati msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Balozi Dkt Emanuell John Nchimbi uliposimama kusalimia wananchi eneo la Usa River Wilaya ya Arumeru Mkoa wa Arusha ukiwa njiani kuelekea Mkoa wa Kilimanjaro.

Chapisha Maoni

0 Maoni