Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj.
Dk. Hussein Ali Mwinyi ameahidi kuendeleza ushirikiano wa muda mrefu uliopo
kati ya Zanzibar na Oman.
Rais Alhaj Dk.Mwinyi amesema hayo leo katika hafla ya futari
iliyoandaliwa na Balozi Mdogo wa Oman
Zanzibar, Mhe.Said Salim Al Sinaw
iliyofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip, Uwanja wa ndege Mkoa wa Mjini
Magharibi jana.
Kwa upande mwingine Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali ya Oman
imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuisaidia Zanzibar katika miradi ya
Maendeleo ikiwemo ukarabati wa majengo ya kihistoria, Afya na Elimu.
0 Maoni