Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kupitia Idara
ya Mawasiliano imeshinda Tuzo ya Umahiri katika Mawasiliano ya Umma iliyobeba
dhima ya “The Best use of Influencers Category for the year 2023”.
Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika usiku wa jana tarehe
05.04.2024 katika Ukumbi wa St. Peter’s jijini Dar es Salaam, tuzo ambazo
zimetolewa na taasisi ya Public
Relations Society of Tanzania (PRST).
Mgeni rasmi katika utoaji wa tuzo hiyo alikuwa Naibu Waziri
wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Maryprisca
Winfred Mahundi.
Ushindi huo umetokana na mchango mkubwa unaotolewa na Idara
ya Mawasiliano ya TANAPA katika kuhabarisha umma masuala mbalimbali ya Uhifadhi
na Utalii.
0 Maoni