Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemuapisha aliyekuwa Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Paul Makonda leo Aprili 4, 2024 Ikulu, Dar es Salaam kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Makonda ameapishwa pamoja na viongozi mbalimbali aliyewateua
Mhe. Rais Samia, wakiwamo Waziri, Manaibua Waziri, Manaibu na Makatibu Wakuu na
Wakuu wa Mikoa katika hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu ya Dar es Salaam.
"Makonda,umefanya kazi nzuri sana kwenye chama,kilikuwa
kimelala umeiamsha sasa watu wanatoka na kujua wajibu wao,umekuwa Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam ulifanya kazi nzuri sana, nimekupeleka Arusha nina imani kubwa
na wewe na unajua kwa nini nimekupeleka pale, kafanye kazi kuusaidia mkoa wa
Arusha, kama unavyojua ni mkoa wa utalii," alisema Rais Samia.
0 Maoni