Taasisi ya Utafiti
wa Wanyamapori Tanzania ( TAWIRI) ni miongoni mwa taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Maliasili
na Utalii zinazoshiriki maonyesho siku ya Misitu Duniani na Siku ya
Upandaji Miti Kitaifa inayoadhimishwa leo 21, Machi 2024.
Akizungumza katika maonesho hayo yanayoendelea Wilayani Same-
Kilimanjaro, Mtafiti kutoka TAWIRI,
Kipemba Ntiniwa amewakaribisha wananchi kutembelea banda la
TAWIRI kujifunza na kupata ushauri wa
tafiti za Wanyamapori na makazi yao ikiwa ni pamoja na Misitu, ufugaji bora wa
Nyuki na uongezaji thamani mazao ya Nyuki.
Ntiniwa ameeleza tofauti na mazao ya nyuki
yaliyozoeleka, kwa sasa TAWIRI imeandaa zao jipya la Asali ya MASEGA ya
Nyuki wakubwa ( COMB HONEY ) ambayo ni
muhimu kwa afya ya Binadamu kwani inasaidia kupunguza “cholesterol” kwenye
damu, kuimarisha kinga za mwili (antioxidant, antifungal na antibacterial),
kusaidia mmeng'enyo wa chakula na kuimarisha msukumo wa damu.
"Asali ya Masega
ina vitamini C, B6, B12, A, E,D na haijafanyiwa uchakataji, haijayeyushwa,
haijachachishwa ipo katika hali yake ya
uhalisia kama ilivyotengenezwa na Nyuki
kwenye masega ndani ya Mzinga, " ameeleza Ntiniwa.
Aidha, Ntiniwa ametoa
wito kwa jamii kutunza Misitu kwani inaumuhimu mkubwa kwa viumbe hai akiwemo
Binadamu, ambapo amebainisha
katika uhifadhi misitu ni makazi ya
Wanyamapori akiwemo Nyuki, Ndege na Wadudu.Pia Miti na mimea mbalimba
iliopo katika Misitu ni chakula cha Wanyamapori. Pia misitu inahifadhi maji na
ni maeneo ya mazalia ya viumbe mbalimbali.
Ikumbukwe, Misitu ni muhimu sana katika udhibiti wa madhara
ya mabadiliko ya tabia ya nchi.


0 Maoni