Tanzania mwenyeji wa Mkutano wa Kimataifa wa Malezi ya Mtoto

 

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dk. Dorothy Gwajima amesema, uimara na uwezo wa kiakili wa mtoto hujengwa kuanzia mwaka sifuri mpaka miaka minane (0-8).

“Makuzi na uslama wa mtoto huanzia tangu akiwa tumboni mwa mama yake. Yanategemea mama huyo ulimlisha nini, ulikuwa unazungumza naye nini na hata baada ya kuzaliwa, mtoto ulimleaje? Hapa ndio tunapata watoto wenye uwezo mkubwa baadaye na taifa linakuwa na wataalamu,” amesema Dk. Gwajima.

Ametoa kauli hiyo leo tarehe 26 Februari 2024, wakati akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya Habari jijini Dar es Salaam, kuhusu Mkutano wa Kimataifa wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto utaofanyika tarehe 11 – 14, Machi 2024, jijini Dar es Salaam.

Dk. Gwajima amewaeleza wahariri kuwa, Rais Samia Suluhu Hassan atakuwa mgeni rasmi na kwamba, utakuwa na ugeni mkubwa utakaojumuisha washiriki zaidi ya 1,100 ambapo, kati yao washiriki 700 wanatoka nje ya Tanzania ikijumuisha nchi za Afrika Mashariki, Afrika, Ulaya na Amerika na zaidi ya washiriki 400 watatoka Tanzania.

“Nchi yetu imepata fursa ya kuandaa mkutano huo kutokana na jitihada na mafanikio kadhaa yaliyopatikana katika kuandaa na kutekeleza Program Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto yaani JPT - MMMAM ya 2021/2022- 2025/2026,” amesema Dk. Gwajima.

Joseph Kulangwa, Mhariri wa Gazeti la Raia Mwema ameishauri serikali kuwa makini na baadhi ya nyumba za ibada ambazo zimekuwa zikiyumbisha makuzi ya watoto.

“Kuna Kanisa liligomea watoto kupata chanjo, chanjo ni sehemu ya usalama wa mtoto. Sasa makanisa kama haya yanaweza kutupeleka siko,” alisema Dk. Gwajima.

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Angela Akilimali ameeleza matarajio ya Watanzani akutokana na mkutano huo.

Hata hivyo ameishukuru serikali kwa juhudu zilizopelekea kupata wasaa wa kuandaa mkutano huo na kwamba, utakuwa na matokeo chanya kwa taifa.

Chapisha Maoni

0 Maoni