Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA jana Februari 03, 2024 imepokea meli kubwa ya watalii wapatao 102 kutoka Uingereza
waliofika katika Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Magofu ya Kilwa kisiwani na
Songo Mnara kwa ajili ya shughuli za utalii kisiwani humo.
Watalii hao wakiongozwa na Kampuni ya Utalii ya Takim
Holidays walipokelewa na kukaribishwa kwa ngoma za asili ya watu wa Kilwa
Kisiwani iitwayo kitupolo ambayo iliwafanya waonekane wakifurahi muda wote.
Ngome ya Mreno, Msikiti mkubwa na mkongwe, Makaburi ya
Malindi na Makutani Palace ni miongoni mwa maeneo yaliyotembelewa na watalii
hao ikiwa ni pamoja na kupata fursa ya kujifunza tamaduni za watu wa Kilwa
kisiwani.
Historia na upekee wa Hifadhi hii ya Magofu ya Kilwa
kisiwani na Songo Mnara imekuwa kivutio kikubwa cha watalii kutoka Kona
mbalimbali za Dunia ambao hutembelea Hifadhi hiyo Karibu Kila Mwaka.
TAWA inatarajia kuendelea kupokea Meli nyingine zaidi katika kipindi cha Mwezi Februari na Machi, 2024, na hii yote ni kutokana na Kazi kubwa iliyofanywa na muongoza watalii "Tour Guide" namba moja Nchini Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
0 Maoni