Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amewasili Kampala
nchini Uganda ambapo anatarajia kushiriki Mkutano wa 27 wa Maspika na Makatibu
wa Mabunge Wanachama wa Jumuiya ya Madola unaofanyika nchini humo kuanzia leo.
Mkutano huu unatarajiwa kuangazia na kutoa fursa kwa Viongozi wa Mihimili kupeana uzoefu na mbinu chanya mpya juu ya hatua mbalimbali za uendeshaji wa Mabunge pamoja na kujenga mahusiano mazuri zaidi yatakayoleta hamasa kwenye kufikia diplomasia ya Kibunge ndani ya Jumuiya hiyo.
0 Maoni