Bodi ya Utalii Tanzania kupitia Mradi wa REGROW imeongoza
watalii 165 wa umoja wa watu wenye usikuvu hafifu kutoka nchi 40 ambapo
wamepata fursa ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mikumi.
Vivutio vya Utalii vya Tanzania vina miundombinu rafiki
inayowawezesha watu wenye mahitaji maalum kuvimbelea na kufurahia uzuri wa
vivutio vya Utalii vya asili vya Tanzania.
Wakiwa hapa nchini wameweza kufanya kongamano pamoja na
kuendesha Mashindano ya Ulimbwende na Utanashati Miss & Mister Deaf
International 2023 ambayo yamefanyika tarehe 25/11/2023 jijini Dar es Salaam.
0 Maoni