NECTA yatangaza matokeo ya darasa la saba

 

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba uliofanyika mwezi Septemba mwaka huu, huku likitangaza kufuta matokeo ya wanafunzi 31 kwa udanganyifu.

Akitangaza matokeo hayo leo Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Said Mohamed amesema ufuaulu wa jumla umepanda kwa asilimia 0.96 na kufikia asilimia 80.6 ambapo watahiniwa 1,092,960 wamefaulu kwa daraja A, B na C.

Dk. Mohamed amesema kwa jumla ya watahiniwa 1,397,395 walisajiliwa kufanya mtihani wa taifa wa darasa la saba, ambapo wanawake ni 742,960 sawa na asilimia 53 na wanaume ni 654,603 sawa na asilimia 47.

Ameongeza kuwa hata hivyo ni watahiniwa 1,356,397 tu ndio waliofanya mtihani wa taifa wa darasa la saba, ambapo wanafunzi 40,901, hawakufanya mtihani huo uliofanyika Septemba 13-14, mwaka huu.

Pamoja na mambo mengine Dk. Mohamed amesema wanafunzi 360 ambao walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mitihani yote, au idadi kubwa ya masomo watarudia mitihani mwaka 2024.

Pata Matokeo Hayo Kwa Kutumia Link Hapo Chini :-

https://matokeo.necta.go.tz/results/2023/psle/index.htm

Chapisha Maoni

0 Maoni