Jeshi la Polisi mkoa wa
Mwanza limebaini mapungufu katika kampuni binafsi za ulinzi ikiwemo walinzi
kutokuwa na sifa ya kufanya kazi hiyo na wamiliki wa makampuni hayo kutopeleka
makato ya michango ya watumishi wao kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.
Zoezi la kukagua makampuni
hayo binafsi katika wilaya ya Ilemela limeongozwa na Afisa Polisi Jamii mkoa wa
Mwanza Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Ramadhan Sarige pamoja na maafisa
wengine wa jeshi hilo.
Kampuni zilizokaguliwa ni
pamoja na West Security Serivices, Intelligence Securico na Masa Security
Services Limited, mara baada ya kuzikagua ACP Sarige akawataka wamiliki wa
kampuni zote za ulinzi kutoa ushirikiano na kuwasilisha nyaraka muhimu wakati
wa ukaguzi huo.
"Nawaagiza wakuu wa
Polisi wilaya OCD's na wakaguzi kata kuhakikisha wanafanya ukaguzi wa kina kwa
kuangalia nyaraka muhimu zinazotakiwa kuwepo kwenye kampuni binafsi za ulinzi
na vitendea kazi vingine kwa mujibu wa sheria," amesema ACP Sarige.
0 Maoni