Kambi maalumu ya upasuaji wa kuweka nyonga na magoti bandia yaanza Mloganzila

 

Kambi maalumu ya upasuaji wa kuweka nyonga na magoti bandia imeanza leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila.

Kambi hiyo inaendeshwa na Prof. Mamoun Gadir kutoka Hospitali ya Queen Elizabeth ya nchini Uingereza, kwa kushirikiana na wataalamu wa Mloganzila.

Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Upasuaji MNH-Mloganzila Dkt. Godlove Mfuko amesema katika siku ya kwanza jumla ya wagonjwa sita wamefanyiwa upasuaji na katika siku tano za kambi watu 35 watanufaika na upasuaji huo.

Aidha, amebainisha kuwa kambi itaendelea hadi Desemba Mosi mwaka huu na baada ya kambi utaratibu wa kawaida wa matibabu hayo utaendelea ambapo wagonjwa wataendelea kuhudumiwa na wataalamu wazalendo.

Chapisha Maoni

0 Maoni