Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema mpaka kufikia
mwaka 2025 atakuwa ameshatimiza ahadi zote alizozitoa wakati wa kampeni ikiwemo
maeneo mazuri ya kufanya biashara, mitaji pamoja na kodi nafuu katika masoko
wanapofanyia biashara zao.
Rais Dk. Mwinyi amesema hayo
wakati alipofungua jengo la wajasiriamali Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini
Pemba leo tarehe 02 Novemba 2023.
Vilevile ameleeza kuwa
shilingi bilioni 31 zilizowekwa na Serikali katika benki ya CRDB wajasiriamali
wameendelea kukopa bila ya riba kwa sababu riba zote zinabebwa na Serikali.
Aidha, Rais Dk.Mwinyi
amewahimiza wajasiriamali waliokuwa kwenye maeneo rasmi waendelee kuomba mitaji
hiyo ya Serikali ambayo haina riba.
Pia ametoa miezi mitatu bure
bila kulipa kodi kwa wajasiriamali wa kituo cha Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba.
0 Maoni