Wanyamapori hai wametajwa kuwa kivutio kikubwa katika
maonesho ya Utalii Mwana Katavi yanayofanyika wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi
kiasi cha kufanya wakazi wa Mkoa huo kufurika katika banda la TAWA ili kupata
maelezo kuhusu tabia na fursa za ufugaji wa Wanyamapori hao.
Maonesho haya ambayo hufanyika Kila mwaka Mkoani humo
yalifunguliwa rasmi Oktoba 25, 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua
Mrindoko ambapo leo Oktoba 31, 2023 yanatarajiwa kufikia tamati.
TAWA imeshiriki na
kutumia maonesho hayo kuhamasisha utalii wa ndani kwa kuwahimiza wakazi wa Mkoa
huo kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo ukanda wa magharibi hususani
bustani ya Wanyamapori hai Tabora almaarufu Tabora ZOO iliyo chini ya Usimamizi
wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).
Wanyamapori waliokuwa kivutio katika maonesho hayo ni Simba,
chui, fisi, Kobe na ndege wa aina mbalimbali ambao walichochea udadisi wa
uelewa kwa wanafunzi wa shule za awali na sekondari waliotembelea banda la TAWA.
TAWA inaendelea kutumia vyema maonesho mbalimbali
yanayofanyika ndani na nje ya nchi yetu kunadi fursa za utalii na uwekezaji
zilizosheheni katika taasisi hii ili kuchangia katika lengo la Serikali
kufikisha idadi ya watalii Millioni Tano (5) ifikapo 2025.
Na Beatus Maganja- Katavi
0 Maoni