Hifadhi ya Taifa Serengeti imeibuka kidedea kwa kuwa mshindi
wa kinyang’anyiro cha Tuzo ya Hifadhi bora barani Afrika kwa mwaka 2023 (Africa’s
Leading National Park 2023) ikiwa ni mara ya tano mfululizo kushinda Tuzo hii.
Hii ni baada ya kuwagaragaza washindani wa tuzo hiyo kama
Central Kalahari Game Reserve- Botwswana, Etosha National Park -Namibia, Kidepo
Valley National Park -Uganda, Kruger National Park -South Africa, pamoja na
Masai Mara National Reserve – Kenya.
Tuzo hiyo imetolewa na ‘World Travel Awards’ usiku wa tarehe
15 Oktoba, 2023 katika hotel ya Atlantis The Royal Dubai, katika nchi za Falme
za Kiarabu na kupokelewa na Mkuu wa
Kanda ya Magharibi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Izumbe Msindai, kwa
niaba ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania ( TANAPA).
0 Maoni