Mshambuliaji wa Liverpool na Misri Mohamed Salah ametoa wito
kwa viongozi duniani kuungana kuzuia mauaji zaidi ya watu wasio na hatia katika
vita inayoendelea ya Israel na Gaza.
Maafisa wa afya wa Gaza wamesema mamia ya watu wameuawa
katika shambulizi lililofanywa kwenye hospitali yenye watu wengi katika mji wa
Gaza Jumanne usiku.
Salah mwenye umri wa miaka 31, amesema misaada ya kibinadamu
kwenda Gaza lazima iruhusiwe mara moja.
“Kumekuwapo na ghazi nyingi, matukio ya kuvunja moyo na
ukatili katika vita hiyo inayoendelea kati ya Isarel na Gaza,” amesema Salah.
0 Maoni