Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.
Hussein Ali Mwinyi ameanza ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo kuelekea
shamra shamra za miaka mitatu ya Serikali ya awamu ya nane madarakani ambapo amefungua
hospitali ya Kivunge baadae aliweka jiwe la msingi katika ujenzi unaoendelea wa
Skuli ya ghorofa Donge Mkoa wa Kaskazini Unguja leo tarehe 23 Oktoba ,2023.
Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali imekuja na utaratibu mpya
wa kushirikisha sekta binafsi katika kutoa huduma kwa hospitali za Serikali
ikiwemo maabara, utoaji wa dawa, huduma za Xray na Ultra sound, chakula pamoja
na usafi lengo ni kutoa huduma bora za kisasa na za haraka kwa wananchi.
Rais Dk. Mwinyi amesema hayo leo wakati akifungua rasmi
Hospitali ya wilaya ya Kivunge, Wilaya ya Kaskazini "A" Mkoa wa
Kaskazini Unguja.
Vilevile Rais Dk. Mwinyi amewahakikishia wananchi Serikali
itaendelea kujenga Skuli za Msingi na Sekondari za Ghorofa kwa pesa ya
Serikali, ujenzi wa barabara, miradi ya maji na miradi ya maendeleo yote kwa
pesa za Serikali.
Rais Dk. Mwinyi amesema wapigaji makelele wachache ni wale
wabadhirifu na mafisadi ambao mirija yao imezibwa kwa sasa Serikali malengo
yake fedha zinakwenda kwenye miradi ya huduma za kijamii, mishahara ya
wafanyakazi wa Serikali, pensheni kwa wastaafu na jamii.
🗓️23 Oktoba 2023
📍Mkoa wa Kaskazini
Unguja.
0 Maoni