Moto umeteketeza bweni la wanafunzi katika shule ya Sekondari
ya wasichana ya Omumwani katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.
Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji mkoa wa Kagera, Zabron Muhumma, amesema kwamba tukio hilo limetokea
jana majira ya saa 2:00 usiku.
Kamanda Mhumma amesema hata hivyo askari wa jeshi hilo
walifanikiwa kuudhibiti moto huo kwa kushirikiana na wananchi na kuepusha
kutokea madhara makubwa.
Moto huo umeteketeza mali, hata hivyo haukusababisha madhara
yoyote kwa binadamu na hadi sasa chanzo chake hakijajulikana, amesema Kamanda Mhumma.
0 Maoni