Mwanamke mashuhuri na balozi wa Taasisi ya Global Women
Wealth Worriors Leaders iliyopo Atlanta Marekani Leo Oktoba 7, 2023 ametembelea
bustani ya Wanyamapori hai iliyopo Mlimani City katika maonesho ya Saba ya
Kimataifa ya Swahili International Tourism Expo (SITE) yanayoendelea Jijini Dar
es Salaam.
Mrs Georgia ambaye ni mlimbwende na mwanamke mwenye
ushawishi mkubwa katika masuala ya uongozi na biashara nchini Marekani ameeleza
kufurahishwa kwake na ubora wa maandalizi ya maonesho ya SITE na kuwaona Wanyamapori
hai mubashara katika maonesho haya.
Pamoja nae Mrs Georgia aliambata na timu ya wamarekani
watano ambapo amewataka wamarekani wote kutembelea bara la Africa hususani Nchi
ya Tanzania kwakuwa ni Nchi yenye utajiri mkubwa wa vivutio vya utalii hasa
rasilimali Wanyamapori na kuahidi kuwa balozi mzuri wa vivutio vya utalii
vilivyopo nchini.
Maonesho ya SITE yanatarajiwa kufikia tamati kesho Oktoba 8,
2023.
Na. Beatus Maganja, Dar es Salaam
0 Maoni