Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akiwa amesimama na Mwenyeji wake Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema
wakati wa Wimbo wa Taifa wa Tanzania na Zambia ukiimbwa mara baada ya kuwasili
kwenye eneo la Mnara wa Kumbukumbu ya Wapigania Uhuru (Mashujaa) wa nchi hiyo
kwenye maadhimisho ya miaka 59 ya Uhuru wa nchi hiyo, Mtaa wa Uhuru Jijini
Lusaka tarehe 24 Oktoba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mwenyeji wake Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema wakati viongozi mbalimbali walipokuwa wakiweka Mashada ya maua kwenye eneo la Mnara wa Kumbukumbu ya Wapigania Uhuru (Mashujaa) wa nchi hiyo katika maadhimisho ya miaka 59 ya Uhuru wa nchi hiyo Jijini Lusaka tarehe 24 Oktoba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka shada la maua kwenye mnara wa kumbukumbu ya Wapigania Uhuru (Mashujaa) Lusaka Zambia tarehe 24 Oktoba, 2023.
Matukio mbalimbali katika maadhimisho ya miaka 59 ya Uhuru wa Taifa la Zambia katika mnara wa kumbukumbu ya Wapigania Uhuru wa Taifa la Zambia uliopo Mtaa wa Uhuru Jijini Lusaka. Zambia inaadhimisha miaka 59 ya Uhuru wa nchi hiyo tarehe 24 Oktoba, 2023.
0 Maoni