Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya
Wadhamini ya Zanzibar Maisha Bora Foundation Mhe. Mama Mariam Mwinyi amewasili Bujumbura,
Burundi kushiriki katika Jukwaa la Wanawake Viongozi kujadili Mchango wa Uzazi
wa Mpango katika kupata Lishe bora na Tija ya Makundi ya watu utakaofanyika
kuanzia tarehe 9 hadi 11 Oktoba 2023.
Mhe. Mama Mariam Mwinyi amepokelewa jana na Kaimu Balozi wa Tanzania
nchini Burundi Joachim Nyingo na Waziri wa Biashara wa Burundi Mhe. Marie
Chantal Nijimbere.
Jukwaa hilo moja ya nyanja za Diplomasia kupitia Wenza wa
Wakuu wa Nchi na Serikali kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya nchi zetu
mbili.
0 Maoni