Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya
wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) Mhe.Mama Mariam
Mwinyi ametoa rai kuwekeza katika elimu ya mtoto wa kike ili kumwezesha
kiuchumi, kijamii husasan kujiamini kufanya maamuzi sahihi kuhusiana na afya ya
uzazi na mpangilio kufikia maendeleo endelevu kwa kuzingatia uzazi wa mpango na
lishe bora kulingana na mahitaji ya idadi ya watu.
Mama Mariam Mwinyi ameyasema hayo jana akitoa salamu za nchi
katika ufunguzi wa Jukwaa la nne la Viongozi Wanawake lililoandaliwa na Mke wa
Rais wa Burundi Mhe. Angeline Ndayishimiye lililofanyika ukumbi wa Hoteli ya
Kiriri, Bujumbura Burundi.
Jukwaa hilo limefunguliwa rasmi na Waziri Mkuu wa Burundi
Mhe.Gervais Ndirakubuca aliyemwakilisha Rais wa Burundi Mhe.Evariste
Ndayishimiye.
Wengine waliohudhuria ni Mke wa Rais wa Kenya Mhe.Mama
Rachel Ruto, Mke wa Rais wa Rwanda Mhe.Mama Jeannette Kagame pamoja na wageni
waalikwa mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa Mashirika ya Umoja wa Afrika,
kikanda, wadau wa maendeleo na ujumbe kutoka China.
0 Maoni