Mama Mariam Mwinyi ashiriki ufungaji wa Jukwaa la Viongozi Wanawake Burundi

 

Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) Mhe.Mama Mariam Mwinyi ameshiriki katika shughuli ya ufungaji wa Jukwaa la nne la Viongozi Wanawake lililoandaliwa na Mke wa Rais wa Burundi Mhe. Mama Angeline Ndayishimiye.

Majadiliano na michango mbalimbali iliwasilishwa na kujadiliwa katika Jukwaa hilo lililojikita kuelewa uwiano baina ya uzazi wa Mpango Usalama wa Chakula, lishe na mgawanyiko wa faida ya kimahitaji kwa makundi ya watu.

Waziri Mkuu wa Burundi Mhe.Gervais Ndirakubuca amefunga rasmi jukwaa hilo jana katika ukumbi wa mikutano Hoteli ya Kiriri, Burundi.

Viongozi wanawake kutoka nchi mbalimbali wameshiriki wakiwemo kutoka Kenya, Rwanda, pia wageni waalikwa mbali mbali wawakilishi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa Afrika na Kikanda pamoja na wadau wa maendeleo na ujumbe kutoka China.

Chapisha Maoni

0 Maoni