Serikali ya kijeshi ya Niger imesema imedhibiti jaribio la kutoroka
nchini la aliyekuwa rais wa nchi hiyo aliyeondolewa madarakani Bw. Mohammed Bazoum.
Rais huyo wa zamani alijaribu kutoroka nchini usiku akiwa na
familia yake, msemaji wa jeshi la Niger amesema.
Ameongeza kwamba kulikuwa na mipango ya kumtorosha rais
Bazoum kwa kutumia helkopta lakini mipango hiyo imegundulika.
Bw. Bazoum amekuwa chini ya ulinzi nyumbani kwake tangu
walinzi wa rais kufanya mapinduzi mwishoni mwa mwezi Julai.
0 Maoni