Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Mhe.Dk. Hussein Mwinyi amesema Tanzania inatekeleza kwa dhati haki za binadamu
na watu na kutoa fursa kwa Wananchi wake kupata haki mbalimbali za binadamu na
watu.
Dk. Mwingi ameeleza hayo jana akifungua Kikao cha 77 cha
Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu uliofanyika ukumbi wa kimataifa wa
Mikutano AICC Jijini Arusha.
Rais Dk. Mwinyi amesema, Serikali zote mbili zinatekeleza
miradi mbalimbali ili kutoa haki za kijamii lakini pia inatoa fursa kwa
Wananchi wake kupata haki kwenye vyombo mbalimbali vya sheria.
Aidha Rais Dk. Mwinyi ametolea mfano uhuru wa kupata habari
unaotokana na wingi wa vyombo vya habari ambavyo kwa sasa vimepatiwa uhuru wa
kufanya kazi zake za kuhabarisha umma bila vikwazo vyovyote.
0 Maoni