Kwa mara ya kwanza, Bodi ya Maktaba ya Tanzania (TLSB), imezindua
chumba cha Maktaba ya watoto katika Hospitali ya rufaa ya Sekou Toure, katika Jiji
la Mwanza.
Akieleza juu ya azma ya kuchukua hatua hiyo, Mkurugenzi Mkuu
wa TLSB Dkt. Mboni Amiri Ruzegea, amesema watoto wanaolazwa Hospitali kwa muda
mrefu, huwa wanakosa kmmahali pa kujifunzia na kucheza. Sasa watakuwa
wakiitumia maktaba hiyo kwa ajili ya kujifunza.
“Hawapoteza muda. Watakuwa wakitibiwa huku wanajisomea, na
kucheza michezo mbalimbali” alisema Dkt. Ruzegea.
Maktaba kuu imetoa vitabu zaidi ya 300, vifaa vya michezo
vya watoto, mazulia na picha mbali mbali.
0 Maoni