Barcelona wameanza na ushindi mkubwa katika mchezo wao wa
kwanza wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, kwa kuichakaza Royal Antwerp magoli matano
kwa bila.
Kikosi hicho cha Xavi, walijikuta wakiongoza kwa magoli
matatu ndani ya dakika 23, yaliyofungwa na Joao Felix na Robert Lewandowski, pamoja
na lakujifunga la Jelle Bataille.
Gavi aliwaongezea Barcelona goli la nne, kabla ya Felix
kufunga goli lake la pili katika mchezo huo na kuwafanya waanze vyema michuano
hiyo.
0 Maoni