Shamra shamra za Wiki ya Simba leo tarehe 4 Agosti 2023
zilihamia Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam baada ya timu hiyo ya mpira
wa miguu kuamua kuweka onesho kuhusu historia yao tangu kuanzishwa kwake mwaka
1936.
Onesho hilo lenye vionjo mbalimbali kuhusu timu hiyo
limenogeshwa na uwepo kioneshwa cha simba mnyama ambaye amehifadhiwa Makumbusho
na Nyumba ya Utamaduni ambaye alitolewa na wamasai kwa Mwl. Julius K. Nyerere,
Rais wa kwanza wa Tanzania kutokana na uongozi bora baada ya kung'atuka mwaka
1985.
Baadhi ya vioneshwa vilivyowekwa kwenye onesho hilo ni
pamoja na makombe ambayo timu ya Simba imewahi kupata katika historia ya mchwzo
wa mpira wa miguu Tanzania ikiwa ni pamoja na kufika hatua ya fainali katika
kombe la Shirikisho la Vilabu barani Afrika (CAF), medali, jezi, picha
mbalimbali na bendera.
Oneaho hili lipo wazi jwa wananchi wote wanaotaka
kutembelea. Tembelea Makumbusho ya Taifa uione Simba.
0 Maoni