Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila ameutaka
uongozi wa Manispaa ya Kinondoni kusimamia vema mchakato wa upatikanaji wa
Viongozi waadilifu wa soko hilo ili kukabiliana na kasoro zilizoko hivi sasa.
RC Chalamila amesema hayo jana alipo zuru
katika Soko hilo kukagua miundombinu na kuongea na wafanyabishara wa Soko hilo
Mhe Mkuu wa Mkoa amebaini kasoro mbalimbali ikiwemo Usalama
hafifu wa Soko, Upangishaji holela ambapo wako baadhi ya watu wasiowaaminifu
hupangisha meza kwa bei ya juu inayokizana na bei halisi ya Serikali pia uwepo
wa miundombinu chakavu ndani ya Soko.
Hata hivyo RC Chalamila amekemea uwepo wa madalali katika
Soko ambao hupandisha bei za Upangishaji wa fremu na meza, kuepuka rushwa, pia
kuimarisha ulinzi shirikishi, na usafi wa Soko pamoja na Viongozi wa mwanzo
kutogombea tena nafasi za uongozi katika Soko hilo wapishe Viongozi wapya.
Aidha RC Chalamila ameagiza TAKUKURU kuwakamata wale wote
wanaohusika na uuzaji wa meza kwa bei ya juu wahojiwe wakikutwa na hatia
wapelekwe mahakamani, pia amewahakikishia wafanyabishara hao kuzimaliza
Changamoto zote katika Soko hilo kwa Kipindi kifupi.
Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Saad Mtambule
amesema soko hilo lina wafanyabishara takribani 883 dhamira ya Manispaa ni
kuboresha Soko hilo, kupata uongozi imara wenye kutetea masilahi ya
wafanyabishara ndio maana tuliamua kuvunja uongozi wa mwanzo na sasa tuko
katika Kipindi cha mpito kupata uongozi mpya wa Soko.
0 Maoni