Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.
Hussein Ali Mwinyi amelipongeza Kanisa la Anglikana Tanzania kwa kuendeleza
amani, umoja na mshikamano nchini.
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo alipokutana na Askofu
Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania Maimbo Mndolwa na ujumbe wake waliofika
Ikulu Zanzibar kujitambulisha baada ya kuchaguliwa mwezi Februari mwaka huu
kuliongoza Kanisa hilo kwa kipindi cha miaka mitano.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi amewashukuru viongozi wa kanisa hilo
kwa mipango yao ya kuitangaza Zanzibar katika sekta ya utalii na Serikali ipo
tayari kuendeleza ushirikiano na kanisa katika sekta hiyo.
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana Tanzania Maimbo Mndolwa
amempongeza Rais Dk. Mwinyi kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwaletea maendeleo
wananchi wa Zanzibar.
Vilevile Askofu Mndolwa amesema kanisa linaendelea kumuombea
katika uongozi wake.
🗓️30 Agosti, 2023
📍Ikulu, Zanzibar.
0 Maoni