Rais Ali Bongo ameonekaka kwa mara ya kwanza kwenye video
aliyotuma tangu kutokea kwa mapinduzi ya kijeshi Gabon, akiwaomba marafiki wa nchi hiyo duniani kote kupaza sauti zao kupinga mapinduzi.
Ali ambaye alikuwa akionekana kama mtu ambaye si rahisi
kutetereka ama kutetemeshwa ameonekana akiwa mnyonge na mpweke.
Katika video hiyo Ali Bongo amesema kuwa anashikiliwa katika
makazi yake, hayupo na mkewe na mtoto wake pia yupo kwingine.
“Sijui kinachoendelea nimeshikiliwa kwenye makazi yangu,
nawaomba marafiki wote tulionao duniani mpaze sauti zenu dhidi ya hiki kinachoendelea, nawaomba mpaze
sauti,” Ali amesema kwenye video hiyo.
Jeshi la nchi hiyo limetangaza kutengua matokeo ya uchaguzi
wa rais ya Jumamosi yaliyompa ushindi rais Ali Bongo, na kuunda kamati ya mpito
ya mabadiliko ya utawala wa nchi hiyo.
0 Maoni