Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila yamsaidia mtoto
mwenye changamoto ya kiafya vifaa vya kumsaidia kupumua.
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kwa kushirikiana na
wahisani imemsaidia vifaa tiba mbalimbali mtoto mwenye changamoto ya ukuaji
kutokana na kusumbuliwa wa Cerebral Palsy hali inayomlazimu kuhitaji uangalizi
wa karibu katika kutatua changamoto za ugonjwa huo.
Mtoto Elisha Kigobanya mwenye umri wa miaka saba alilazwa
hospitali hapa takriabni miezi 11 kutokana na tatizo hilo linalomkabili, leo
Agosti 15, 2023 ameruhusiwa kurudi nyumbani baada ya kupata nafuu.
Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo kwa wazazi wa
Elisha, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Mloganziala Dkt. Julieth Magandi
ameeleza kufurahishwa na maendeleo ya kiafya ya mtoto huyo na kuahidi kuwa
hospitali itaendelea kuwa bega kwa bega katika kutoa ushauri wa kitabibu pale
itakapo hitajika.
"Ni jambo la kushukuru kuona afya ya mtoto Elisha
inaendelea kuimarika na sasa ameruhusiwa, nachukua nafasi hii kueleza kwamba pamoja
na wahisani wengine kutoa msaada wa godoro hewav (air mattress) pamoja na
kitanda uongozi wa hospitali tumempatia msaada wa vifaa vya Oxygen Concentrator
na Nebulizer mashine ambavyo atatumia kwa muda mpaka pale atakapokua havihitaji
tena, " amesema Dkt.a Magandi
Kwa upande wake Baba mzazi wa Elisha, Bw. Kenneth Kigobanya
ameushukru uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kwa ukarimu,
upendo, matibabu na huduma zote za kiutu walizozitoa kwa mtoto wao tangu
alipopokelewa hospitalini Septemba 2022.
"Kipekee napenda kuushukru uongozi na watumishi wa
Mloganzila kwa namna walivyopambana na kuhakikisha wanaokoa maisha ya mwanangu
ambaye awali hali yake kiafya ilikua mbaya,’’ ameeleza Bw. Kigobanya.
@muhimbili_taifa
@elisha_ecpft
0 Maoni