Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amechaguliwa muhula wa
pili kwa ushindi wa asilimia 52.6 za
kura, tume ya uchaguzi ya nchi hiyo imesema.
Hata hivyo upinzani nao umedai kushinda uchaguzi huo,
ukisema kumekuwapo na udanganyifu mkubwa wa kura, huku waangalizi wakisema
uchaguzi huo haukukidhi viwango vya demokrasia.
Mnangagwa maarufu kwa jina la Mamba ni rais wa tatu wa nchi
hiyo, ambaye aliingia madarakani mwaka 2017 kufuatia mapinduzi dhidi ya Robert Mugabe.
Wananchi wa Zimbabwe bado wanakabiliwa na mfumuko mkubwa wa
bei, umasikini pamoja na hofu ya mabadiliko ya hali ya hewa.
0 Maoni